Makosa Madogo Madogo TRA Katika Kubadili Umiliki.

Watu wengi hujiandaa kwenda TRA wakiwa na imani kuwa kubadili umiliki ni mchakato rahisi mradi tu wana fedha na nyaraka chache. Lakini uhalisia ni kwamba watu wengi hurudishwa TRA na kuishia kupoteza muda! Na si kwa makosa makubwa, bali kwa makosa madogo madogo ambayo yangeweza kuepukika kama yangejulikana mapema. Baadhi ya makosa hayo ni:

  • Mkataba wa mauziano ambao hauja gongwa muhuri na mwana sheria.
  • Mkataba wa mauziano ambao hauna risiti ya EFD.
  • Mkataba wa mauziano wenye risiti ya EFD isiyosoma katika mfumo wa TRA Verify.
  • Kutokua na Tax Clearence kwa chombo cha moto cha biashara
  • Mmiliki wa awali kuwa na deni la kodi katika chombo cha biashara alicho uza.
  • Kutokua na TIN namba sahihi na active mmiliki wa awali au mmiliki mpya.
  • Kutokua na “Certificate of Gift” kwa chombo ambacho kilitolewa kama zawadi au urithi au kwa njia nyingine tofauti na mauziano. Ni lazima mmiliki wa zamani ampe mmiliki mpya “certificate of gift”. Cheti hiki kitasimama kama mkataba, hivyo kisainiwe na pande mbili, mwanasheria agonge muhuri na aweke risiti ya EFD.

Nyaraka Muhimu.

Kubadili umiliki TRA hakuanzii TRA, bali huanza kwa kua na nyaraka sahihi. Watu wengi kucheleweshwa si kwa sababu hawakuwa na fedha, bali kwa sababu walikosa nyaraka moja tu muhimu. Ndiyo maana ni muhimu kabla ya kuanza safari ya TRA andaa nyaraka hizi muhimu:

 

Kwa Chombo Cha Moto – Binafsi

  • Mkataba wa mauziano wenye sifa zote. (Sahihi, Muhuri na EFD risiti ya mwanasheria)
  • TIN za pande mbili.

Kwa Chombo Cha Moto Cha – Biashara

  • Mkataba wa mauziano wenye sifa zote. (Sahihi, Muhuri na EFD risiti ya mwanasheria)
  • TIN za pande mbili.
  • Tax Clearence Certificate
 
Ikiwa nyaraka zako ziko tayari, tunaweza kukufanyia mchakato mzima wa kubadili umiliki online, hadi TRA itoe control number  Bofya Hapa. 

Madhara Kuto-kubadili Umiliki Kwa Wakati.

Kupuuza kubadili umiliki wa chombo cha moto baada ya mauzo si kosa dogo. Madhara yake huonekana baadaye, na mara nyingi huwakuta wahusika wakiwa tayari wamechelewa kujikinga.

Madhara haya huathiri pande zote mbili kama ifuatavyo:


1.Madhara Kwa Mmiliki wa Zamani.

  • Faini na makosa ya barabarani yanayofanywa na mmiliki mpya’
  • Kisheria atahusishwa na ajali zote zitakazotokea.
  • Kodi, na madeni ya TRA yanayoendelea kusajiliwa kwa jina lake.
  • Usumbufu wa kuitwa vituo vya polisi au TRA kujieleza kwa makosa asiyoyafanya

Kwa kifupi jina lako linaendelea kubeba mzigo wa gari ambalo hulimiliki tena.


2. Madhara Kwa Mmiliki Mpya.

  • Kupoteza haki ya kisheria endapo kwa sababu si mmiliki halali.
  • Kukwama wakati wa kuuza tena chombo hicho au kukitumia kama dhamana.
  • Kushindwa kusajili bima mpya kwa jina lake.
  • Kupata shida wakati wa ukaguzi wa polisi barabarani.
 

Kubadili umiliki si hiari na si jambo la kuahirisha. Ni hatua ya mwisho ya mauzo inayolinda pande zote mbili dhidi ya hasara, lawama na matatizo ya baadaye. Kama una nyaraka zote tayari na hutaki kuingia kwenye hatari hizi, tunaweza kushughulikia mchakato mzima wa kubadili umiliki online hadi TRA itoe control number.

Tuta-shughulikia TRA Kwa Niaba Yako.

Kama umekamilisha nyaraka zote, tuta-kufanyia mchakato wa kubadili umiliki, mpaka mwisho hadi TRA watume control number kwa ajili ya malipo. Huduma hii ni salama kwa sababu:

  • Hakuna malipo ya awali! Utatulipa TSh 20,000/= baada ya TRA kutuma control namba . Control Namba ni ishara kwamba mchakato wako umefikia hatua ya mwisho.
  • Baada ya mmiliki mpya kulipia control namba ya TRA, kadi mpya itakua tayari papo hapo!, ikisoma majina ya mmiliki mpya na ukihitaji tutaifwatilia na kukutumia kadi hiyo BURE. 
  • Bofya kitufe cha WhatsApp hapa chini kuwasiliana nasi. Utatuma nyaraka zote muhimu kama ilivyo ainishwa hapa. Kisha tutaanza mchakato rasmi.
  • Kwa kawaida mchakato huu huchukua siku 1-2 za kazi kukamilika. Kadri utakavyotutumia nyaraka zote mapema na ndivyo mchakato uta-kamilika mapema.