Magari Dar es salaam Yanauzwa

Loading

Filters

Results Clear all

Mkoa

Mkoa

Make

Make

Model

Model

Usajili

Usajili

Body-Type

Body-Type

Condition

Condition

Drive Type

Drive Type

Transmission

Transmission

Fuel Type

Fuel Type

Cylinders

Cylinders

Color

Color

Doors

Doors

Safety

Safety
Clear all
More filters
25 Results
Audi A3 2025 Namba D
1,500,000Tsh - Juni 24, 2025
Audi A3 2005 Namba D
20,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Audi A3 2025 Namba D
160,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Audi A3 2012 Namba D
20,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Toyota IST 2007 Namba D
14,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Toyota IST 2005 Namba C
10,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Audi A3 2015 Namba D
50,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Toyota Passo 2005 Unregistered
14,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Toyota IST 2007 Namba D
23,000,000Tsh - Juni 24, 2025
Toyota IST 2005 Namba D
18,000,000Tsh - Juni 22, 2025
Toyota Coaster 2013 Namba D
66,000,000Tsh - Juni 22, 2025
Toyota IST 2002 Namba E
9,000,000Tsh - Juni 22, 2025

Magari Dar es Salaam Yanauzwa: Aina, Bei na Ushauri

Soko la magari Dar es Salaam limekua kwa kasi miaka ya karibuni. Takwimu za hivi majuzi zinaonyesha mauzo ya magari Tanzania yaliongezeka kwa 45.8% mwaka 2024 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia. Toyota imekuwa chapa inayoongoza sokoni (ikifuatiwa na Isuzu na Nissan) kutokana na uimara wake. Tovuti za habari pia zinaonyesha Toyota ikishika nafasi ya juu Tanzania na Nissan, Subaru, Mercedes Benz nazo zikiwa maarufu. Sekta pia inaelekea kupenda magari makubwa ya aina ya SUV kutokana na uimara wao barabarani. Aidha, magari ya kielektriki na ya kuunganisha mafuta (hybrid) yanatazamiwa kuongezeka – Tanzania ni miongoni mwa nchi tano Africa zinazokua katika matumizi ya magari ya umeme. 

 

Aina za Magari Dar es salaam Na Bei

Soko la Dar es Salaam linatoa aina nyingi za magari kulingana na mahitaji na bajeti. Zifuatazo ni aina kuu za magari na viwango vya bei vinavyopatikana Dar es Salaam:

  • Magari Ndogo (Bei Nafuu) – Hizi ni magari madogo yenye ufanisi wa mafuta na bei rahisi, mazuri kwa jiji. Mifano maarufu ni Toyota IST (bei ya TZS 8–19 milioni Toyota IST used) na Toyota Vitz  (bei ya TZS 5 –12 milioni). Magari haya ya bei poa Dar es Salaam yanapendwa kwasababu yana gharama ndogo za ununuzi na matengenezo.
  • Magari ya Kawaida (Sedan) – Sedani kama Toyota Premio (bei 8–15M TZS) na Nissan Sentra (10–18M TZS) huaminika na familia kwa uhakika na vyumba vya kutosha. Kiwango cha chini cha matengenezo na uimara hufanya sedani kuwa chaguo bora kwa safari za kila siku.
  • SUV (Sport Utility Vehicle) – Magari ya aina hii yanapatikana kwa wingi Dar es Salaam. Mfano ni Toyota RAV4 (bei 15–25M TZS) na Subaru Forester (18–30M TZS) kwa magari mapana ya familia. Kwa safari za mbali au barabara mbovu, Toyota Land Cruiser Prado (25–40M TZS) hujivunia nguvu na uimara. Kwa hivyo SUV ni chaguo la wale wanapenda adventure na nafasi kubwa ndani.
  • Magari ya Biashara (Commercial/Pickup) – Haya ni magari imara yanayoweza kubeba mizigo au abiria wengi. Mfano ni Nissan Pickup (Bei kati ya 20 – 30M TZS), Toyota Hilux ( Bei kati ya 25–40M TZS) na Isuzu D-Max (22–35M TZS). Magari haya yanapendwa na wafanyabiashara na sekta ya ujenzi kwa uwezo wao wa kazi nzito na huduma za kila siku.
  • Magari ya Kifahari (Luxury) – Kwa wale wanaotafuta comfort ya hali ya juu, magari kama Mercedes Benz E200 (bei kati ya 30–50M TZS), Toyota Alphard ( bei kati ya 25–60M TZS) na Land Rover Defender (Bei 50–100M TZS) yanapatikana sokoni. Magari haya ni ya gharama kubwa lakini yanakuja na teknolojia ya kisasa na ya hadhi ya juu.

Kwa upande wa magari mapya kwenye showroom Dar es salaam, bei zinaanzia kati ya TZS 25 milioni hadi 200 milioni kulingana na brand na sifa za gari. Kwa mfano, Toyota RAV4 Hybrid showroom Dar es Salaam huanza takribani TZS 125 milioni, Land Cruiser Prado mpya karibu TZS 181 milioni, na Land Cruiser 300 mpya zinauzwa takribani TZS 463 milioni. Hata magari madogo kama Used Toyota Rumion yanagharimu kuanzia takribani TZS 22 milioni, na used Hilux takribani TZS 91 milioni. Mifano hii inaonyesha wazi kuwa bei za magari mapya (kutoka showroom) Dar es Salaam ni kubwa kulinganisha na bei za wauzaji binafsi wa magari used.

 

Magari Mapya vs Used Dar es salaam

Kununua gari mpya kutoka showroom na gari used kuna faida na hasara zake. Magari mapya (0km) hutolewa na warrant ya mtengenezaji, huja na teknolojia mpya na ubora wa hali ya juu, hivyo mtumiaji anapata uhakika kwa muda mrefu. Hata hivyo, bei zake huwa kubwa – gharama za ushuru na kodi zinaweza kufanya thamani ya gari iongezeke mara mbili ikilinganishwa na bei ya awali. Kwa mfano, gari mpya kama Toyota Land Cruiser 300 mpya (0km) ikilipiwa ushuru bei ya huanzia karibu $185,000 (karibu TZS 464 milioni) kwenye showroom, huku gari hilo hilo kablya ya ushuru lingeuzwa bei ya $112,000 ( ≈ TSZ 261M).

Kwa upande mwingine, magari used Dar es Salaam hupatikana kwa bei poa. Zipo gari nzuri kuanzia Tsh 5,000,000/=  hadi Tsh 50,000,000/=  pekee. Hii inaruhusu mnunuzi wa bajeti ndogo kuingia sokoni, hasa wakilenga magari madogo ya familia na SUV za zamani ambazo bado zipo kwenye hali nzuri. Gharama ya chini ya ununuzi ni faida kuu lakini  ukosefu wa  warrant na uhakika wa perfomance ya gari pamoja na historia ya gari. Kwa mfano, Magari used yanaweza kuwa na matatizo ya awali yasiyotambuliwa bila uchunguzi wa kina. Kwa hivyo, kabla ya kununua magari used Dar es Salaam inashauriwa kufanya ukaguzi wa kina wa injini na historia yake.

 

Brand Za Magari Maarufu Dar es Salaam

Brand zinazopendwa Dar es Salaam ni zile za Japan kutokana na uimara na upatikanaji mzuri wa vipuri . Taarifa zinaonyesha Toyota inaongoza kwa kupendwa kutokana na uimara wake na urahisi wa upatikanaji wa vipuri. Wauzaji wa magari  wanataja Toyota, Nissan, Lexus, Mazda, Mitsubishi na Subaru kama chapa kuu zinazopendwa sokoni. Kwa mfano, Toyota Hilux, Land Cruiser na RAV4 zinajulikana kwa kustahimili vizuri mazingira magumu; Nissan X-Trail na Note ni maarufu kwa matumizi mijini; Honda Fit (Jazz) ni chaguo la wakazi wa Dar es salaam kwa ufanisi wake wa mafuta; na Subaru Forester ina perfomance nzuri barabarani. Kampuni hizi zinalenga kutoa magari imara na perfomance, hivyo kufanya Brand hizi kuaminika kwa wanunuzi wa magari Tanzania.

Ushauri kwa Wanunuzi wa Magari

Unaponunua gari Dar es Salaam, kuna mambo muhimu ya kuzingatia ili kufanya ununuzi salama na bora:

  • Bajeti na Mahitaji Yako – Weka wazi kiwango cha pesa unachotaka kutumia na matumizi ya gari. Magari ndogo kama Toyota Ist, Passo Vitz au Suzuki Swift ni bora kwa matumizi ya mjini kwa kuwa hujiona gharama kubwa za mafuta na matengenezo. Kwa safari za mbali au barabara mbovu, ukihitaji nafasi na nguvu zaidi, bifu la SUV kama RAV4 ni zaidi.
  • Kilomita za Gari – Hakikisha unalenga gari kuwa na kilomita (milage) ndogo iwezekanavyo. Kilomita ndogo inaashiria kuwa gari limetumika kidogo, na uwezekano mdogo wa kuwa na matatizo makubwa ya engen. Epuka magari yenye kilomita nyingi sana bila historia kamili ya matengenezo.
  • Hali ya Injini na Matengenezo – Hakikisha injini inafanya kazi bila mlio wa kugonga, hakikisha hakuna engen warning, na ukague maeneo muhimu kama mfumo wa breki na gia. Magari yaliyotunzwa vizuri yana historia ya service na ubadilishwaji wa vipuri kwa wakati. Inapendekezwa kupeleka gari husika kwa fundi wa magari (au auto-mechanic) kabla ya kununua ili kupima hali ya injini na sehemu nyingine.
  • Historia ya Gari – Chunguza kama gari limepata ajali kubwa au limefanyiwa matengenezo makubwa. Hakikisha jina la mmiliki kwenye vyeti vinaendana na mmiliki anaeuza na kwamba gari lina taratibu halali za usajili. Magari mengi mara nyingi huwa na rekodi ya huduma (service book) iliyojazwa kikamilifu.
  • Ufanisi wa Mafuta – Gari lenye ufanisi mzuri wa mafuta litakupunguzia gharama za uendeshaji. Kwa mfano, Toyota RAV4 Hybrid inaonyesha matumizi ya takribani 6.5L kwa 100km, ikilinganishwa na SUV za kawaida zinazotumia mafuta zaidi. Chunguza matumizi ya mafuta ya gari unayochagua na ukadirie gharama za matumizi yako kwa mwaka kulingana na umbali unaotarajia kutembea na bei za mafuta sasa.
  • Tafuta Wauzaji Wa Magari Wanaoaminika – Matangazo ya magari Dar es Salaam yanaweza kupatikana kwenye tovuti kama hapa GariPesa, ambazo zinawaunganisha wanunuzi na wauzaji wa Magari. Fanya utafiti kupitia tovuti yetu ili kulinganisha bei na kupata maelezo zaidi. 

Soko la magari Dar es Salaam lina magari mengi, kuanzia magari bei nafuu Dar es Salaam kama Toyota IST na Vitz zinazopatikana kwa takriban milioni chache za kitanzania, huku magari mapya yenye sifa za kisasa yakipatikana kwa bei ghali kidogo. Kabla ya kufanya ununuzi, angalia kwa makini bei, sifa za gari, na ulinganishe magari mbalimbali. Kwa kufanya hivyo, utaweza kupata gari litakalokidhi mahitaji yako bila kuingia gharama kubwa zisizotarajiwa.

Largest Online Car Market in Tanzania
Copyright © 2025. All rights reserved.