Soko la magari Dar es Salaam limekua kwa kasi miaka ya karibuni. Takwimu za hivi majuzi zinaonyesha mauzo ya magari Tanzania yaliongezeka kwa 45.8% mwaka 2024 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia. Toyota imekuwa chapa inayoongoza sokoni (ikifuatiwa na Isuzu na Nissan) kutokana na uimara wake. Tovuti za habari pia zinaonyesha Toyota ikishika nafasi ya juu Tanzania na Nissan, Subaru, Mercedes Benz nazo zikiwa maarufu. Sekta pia inaelekea kupenda magari makubwa ya aina ya SUV kutokana na uimara wao barabarani. Aidha, magari ya kielektriki na ya kuunganisha mafuta (hybrid) yanatazamiwa kuongezeka – Tanzania ni miongoni mwa nchi tano Africa zinazokua katika matumizi ya magari ya umeme.
Soko la Dar es Salaam linatoa aina nyingi za magari kulingana na mahitaji na bajeti. Zifuatazo ni aina kuu za magari na viwango vya bei vinavyopatikana Dar es Salaam:
Kwa upande wa magari mapya kwenye showroom Dar es salaam, bei zinaanzia kati ya TZS 25 milioni hadi 200 milioni kulingana na brand na sifa za gari. Kwa mfano, Toyota RAV4 Hybrid showroom Dar es Salaam huanza takribani TZS 125 milioni, Land Cruiser Prado mpya karibu TZS 181 milioni, na Land Cruiser 300 mpya zinauzwa takribani TZS 463 milioni. Hata magari madogo kama Used Toyota Rumion yanagharimu kuanzia takribani TZS 22 milioni, na used Hilux takribani TZS 91 milioni. Mifano hii inaonyesha wazi kuwa bei za magari mapya (kutoka showroom) Dar es Salaam ni kubwa kulinganisha na bei za wauzaji binafsi wa magari used.
Kununua gari mpya kutoka showroom na gari used kuna faida na hasara zake. Magari mapya (0km) hutolewa na warrant ya mtengenezaji, huja na teknolojia mpya na ubora wa hali ya juu, hivyo mtumiaji anapata uhakika kwa muda mrefu. Hata hivyo, bei zake huwa kubwa – gharama za ushuru na kodi zinaweza kufanya thamani ya gari iongezeke mara mbili ikilinganishwa na bei ya awali. Kwa mfano, gari mpya kama Toyota Land Cruiser 300 mpya (0km) ikilipiwa ushuru bei ya huanzia karibu $185,000 (karibu TZS 464 milioni) kwenye showroom, huku gari hilo hilo kablya ya ushuru lingeuzwa bei ya $112,000 ( ≈ TSZ 261M).
Kwa upande mwingine, magari used Dar es Salaam hupatikana kwa bei poa. Zipo gari nzuri kuanzia Tsh 5,000,000/= hadi Tsh 50,000,000/= pekee. Hii inaruhusu mnunuzi wa bajeti ndogo kuingia sokoni, hasa wakilenga magari madogo ya familia na SUV za zamani ambazo bado zipo kwenye hali nzuri. Gharama ya chini ya ununuzi ni faida kuu lakini ukosefu wa warrant na uhakika wa perfomance ya gari pamoja na historia ya gari. Kwa mfano, Magari used yanaweza kuwa na matatizo ya awali yasiyotambuliwa bila uchunguzi wa kina. Kwa hivyo, kabla ya kununua magari used Dar es Salaam inashauriwa kufanya ukaguzi wa kina wa injini na historia yake.
Brand zinazopendwa Dar es Salaam ni zile za Japan kutokana na uimara na upatikanaji mzuri wa vipuri . Taarifa zinaonyesha Toyota inaongoza kwa kupendwa kutokana na uimara wake na urahisi wa upatikanaji wa vipuri. Wauzaji wa magari wanataja Toyota, Nissan, Lexus, Mazda, Mitsubishi na Subaru kama chapa kuu zinazopendwa sokoni. Kwa mfano, Toyota Hilux, Land Cruiser na RAV4 zinajulikana kwa kustahimili vizuri mazingira magumu; Nissan X-Trail na Note ni maarufu kwa matumizi mijini; Honda Fit (Jazz) ni chaguo la wakazi wa Dar es salaam kwa ufanisi wake wa mafuta; na Subaru Forester ina perfomance nzuri barabarani. Kampuni hizi zinalenga kutoa magari imara na perfomance, hivyo kufanya Brand hizi kuaminika kwa wanunuzi wa magari Tanzania.
Unaponunua gari Dar es Salaam, kuna mambo muhimu ya kuzingatia ili kufanya ununuzi salama na bora:
Soko la magari Dar es Salaam lina magari mengi, kuanzia magari bei nafuu Dar es Salaam kama Toyota IST na Vitz zinazopatikana kwa takriban milioni chache za kitanzania, huku magari mapya yenye sifa za kisasa yakipatikana kwa bei ghali kidogo. Kabla ya kufanya ununuzi, angalia kwa makini bei, sifa za gari, na ulinganishe magari mbalimbali. Kwa kufanya hivyo, utaweza kupata gari litakalokidhi mahitaji yako bila kuingia gharama kubwa zisizotarajiwa.