Kubadili Umiliki wa Gari TRA

Baada ya kuuza gari, kazi haishi pale tu unapokabidhi funguo na kupokea pesa. Ni muhimu sana kuhakikisha umebadili umiliki wa gari TRA kutoka kwako kwenda kwa mmiliki mpya. Hii itakulinda dhidi ya matatizo ya kisheria au makosa ya baadaye yanayoweza kufanywa na mmiliki mpya. 

 

TRA wameleta mfumo mpya wa kubadilisha umiliki wa vyombo vya moto unaofahamika kama IDRAS. Katika mfumo huu kila kitu hufanyika online. 

 

Mchakato huu wa kubadili umiliki wa gari ni lazima ufanyike na mmiliki halali wa gari (yule anaeuza gari, ambae jina lake na TIN vipo katika kadi ya gari). Hii ni kwa sababu umiliki wa gari bado unakua umeshikanishwa katika TIN ya muuzaji wa gari hili.

 

Ikiwa wewe ni mnunuzi wa gari na unataka kubadilisha umiliki gari ulilo nunua,  ni LAZIMA umshirikishe muuzaji wa gari ili aweze kuingia katika akaunti yake ya Taxpayer Portal na kubadili umiliki wa gari kutoka kwenye TIN yake kuja kwenye TIN yako.

 

 Hapa kuna hatua muhimu za kufuata:

 

1. Andaa Nyaraka Muhimu

Kabla ya kuingia katika mfumo wa IDRAS, hakikisha unakuwa na nyaraka zifuatazo:

  • Kopi ya mkataba wa mauziano uliosainiwa na pande mbili kisha kugongwa muhuri ulioambatana na risiti ya EFD kutoka kwa mwanasheria.
  • TIN za pande mbili, muuzaji na mnunuzi wa gari.
  • Uwezo wa ku-login katika TIN ya Muuzaji na Mnunuzi.
  • Ada ndogo ya uhamisho wa umiliki wa gari (Mara nyingi hulipwa na mnunuzi)

Kuwa na nyaraka hizi kutarahisisha mchakato.

 

2. Login katika mfumo wa TRA Taxpayer Portal 

Kupitia TIN ya mmiliki wa gari (Muuzaji wa gari) login katika Tax payer Portal. Baada ya kulogin Bofya “Services” kisha shuka chini kabisa na bofya “Motor Vehicle & Driving Licence ” . Hapo utapelekwa moja kwa moja katika mfumo wa IDRAS.

 

3. Jaza Taarifa Sahihi Kisha

Baada ya kuingia katika mfumo wa IDRAS hakikisha unajaza taarifa zenu kwa usahihi. Taarifa kama TIN, majina ya mnunuzi na maelezo yote ya gari lazima yaandikwe kwa usahihi. Baada ya kujaza taarifa zote bofya “submit” ili kutuma maombi yako.

 

ANGALIZO: Kujaza taarifa kwenye mfumo huu kunahitaji uelewa wa kitaalamu. Ili kuokoa muda wako na kuondoa usumbufu unaweza kutuachia sisi tukufanyie kila kitu kwa gharama ndogo tu. Tupigie +255763017461 popote Tanzania.

 

4. Lipa Ada ya Uhamisho

Baada ya ku”submit” taarifa zako online katika mfumo wa IDRAS, utapata “Control Namba” ya kulipia ada ndogo ya kubadili umiliki wa gari ambayo baada Control Namba kulipiwa, ada hiyo itaenda moja kwamoja TRA. Gharama ya Ada hii inategemea aina na thamani ya gari. 

Ushauri: Gharama ya Ada hii mara nyingi hulipwa na mnunuzi (Mmiliki Mpya), lakini ni vizuri kukubaliana mapema kabla ya kwenda TRA.

 

5. Pokea Uthibitisho wa Uhamisho

Baada ya “Control Namba” kulipiwa papo hapo mnunuzi atapokea ownership card mpya yenye jina lake katika TIN yake katika akaunti yake ya Tax Payer Portal. Hapa ni rasmi sasa mnunuzi ndie mmiliki mpya wa gari hili.

 

6. Futa Taarifa Zako Kwenye Bima na Road License

Baada ya uhamisho, wasiliana na kampuni ya bima na mamlaka za road license ili kuhakikisha huna tena majukumu yoyote ya kisheria kwa gari hilo. Pia itamsaidia mnunuzi mpya kuweza kuweka bima mpya kwa jina lake.

 

Hitimisho

Kubadili umiliki wa gari ni hatua muhimu ya mwisho baada ya mauzo. Usipuuzie. Kwa kufuata hatua hizi, utalinda jina lako na kuepuka matatizo ya baadaye kama faini, ajali au makosa ya barabarani yanayoweza kufanywa na mmiliki mpya. 

Je, Unayajua Maswali Wanunuzi Wa Magari Huuliza?

Wauzaji wengi hushindwa kuyajibu na kuishia kukosa mteja! GariPesa Tumekuandalia muongozo na majibu sahihi yatakayo mteka mteja wako.

Muongozo huu muhimu, tunakutumia moja kwa moja kwenye WhatsApp na Email yako. Jaza fomu hii sasa.